Na Walter Mguluchuma , Katavi yetu Blog
WANAFUNZI wa Kidato cha Sita Shule ya Sekondari Usevya , Halamshauri
ya Mpimbwe wilayani Mlele katika mkoa wa Katavi wanadaiwa
kuwashambulia kwa kuwacharaza viboko walimu wao wawili miongoni
WANAFUNZI wa Kidato cha Sita Shule ya Sekondari Usevya , Halamshauri
ya Mpimbwe wilayani Mlele katika mkoa wa Katavi wanadaiwa
kuwashambulia kwa kuwacharaza viboko walimu wao wawili miongoni
mwao akiwa Makamu Mkuu wa Shule hiyo , Makonda Ng’oka “Membele
‘(34)ambaye amengolewa meno yake matano .
Inadaiwa kuwa wanafunzi wa kidato cha sita shuleni hapo hawamtaki
Makamu Mkuu wa Shule hiyo kuendelea kufundisha shuleni hapo
kutokana kile wanacho dai kuwa na tabia yake ya kuwadhalilisha wanafunzi wa kiume
shuleni hapo.
Mwezi Mei mwaka huu Ng’oka “Membele” amefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Mpanda kwa tuhuma za kumlawiti mwanafunzi wake kidaiwa kutenda
kosa hilo kati ya Novemba 2015 na April mwaka huu
Inadaiwa kuwa kukamatwa na kufikishwa mahakamani kwa Makamu Mkuu huyo
wa shule hiyo kulifuatia wanafunzi wa kiume wanaosoma Kidato cha Tano
sasa wako Kidato cha Sita katika shule hiyo kumkataa na kutishia
kuandamana kupinga vitendo vyake vya kuwalawiti wanafunzi wake.
Wanafunzi hao walidai kuwa mwalimu huyo amekuwa akiwalawiti baadhi yao
ikiwa ni adhabu mbadala wanapobainika kufanya makosa shuleni hapo.
Hata hivyo baada ya kutopatikana ushahidi wa kumtia hatiani
Mwalimu Makonda ambapo Julai 27 mwaka huu Mahakama ya Hakimu
Mkazi ya Wilaya ya Mpanda ilimwachia huru .
Inadaiwa kuwa baada ya mahakama hiyo kumwachia huru Mwalimu
Makonda aliripoti kwenye kituo chake cha kazi , Shule ya
Sekondari Usevya , Agosti Mosi mwaka huu ambapo kurejea kwake
shuleni hapo kunadaiwa kuamsha hasira kwa wanafunzi wa Kidato cha
Sita wakidai hawapo tayari kumwona mwalimu huyo na familia yake
shuleni hapo .
Akiongea na wanahabari jana mjini hapa Ng’oka alidai kuwa hayuko
tayari kuendelea kufundisha kwenye shule hiyo kwa kuhofia
usalama wake kutoka na kipigo alichokipata cha kushambuliwa na
baadhi ya wanafunzi wake wa kidato cha tano na cha sita wakati
akiwa nyumbani kwake na familia yake .
Akisimulia mkasa huo alisema siku hiyo ya tukio , Agosti 12
mwaka huu alikuwa nyumbani kwake shuleni hapo pamoja na
familia yake pamoja na mwalimu mwenzake aitwae, Gabriel
Kambona aliyekuwa amemtembelea ..
“ Ghafla, saa mbili usiku nikiwa maliwatoni nikioga lilitokea
kundi la wanafunzi wa kidato cha tano na sita wakiwa na silaha za
jadi kama vile fimbo , malungu , mawe na matofali na kuanza
kuishambulia familia yake pamoja na mwalimu Kambona” alieleza
Alidai kuwa alilazimika ‘kuchomoka’ bafuni baada ya kusikia mayowe
yaliyokuwa yakipigwa na familia yake wakiomba msaada ambapo
alipofika sebuleni alishuhudia wanafunzi hao wakiishamulia familia
yake .
“Ndipo walinigeukia na kuanza kunishamubulia kwa kunipiga kwa
marungu na fimbo hadi nikapoteza fahamu nilizinduka nikiwa
nimelazwa kwenye Kituo cha Afya Usevya na kubaini kuwa nimepoteza
meno yangu matano huku nikiwa nimejeruhiwa kichwani ….
. baadae nilihamishiwa katika Hospitali ya Wilaya ya Mpanda
ambako nililazwa wiki moja na nusu kwa matibabu na sasa nimepewa
rufaa niende Hospitali ya Taifa Muhimbili Jijini Dar kwa matibabu
zaidi” alieleza
Alidai kuwa uhasama baina yake na wanafunzi hao umedumu kwa
muda mrefu lakini anashangaa uongozi wa Halmashauri ya Mpimbwe
na Wilaya ya Mlele umeshindwa kumpangia kituo kingine cha
kazi .
“Isitoshe uongozi wa Halmashauri ya Mpimbwe na wa wilaya ya
Mlele haujawachukulia hatu yeyote wanafunzi hao licha ya
kupeleka majina yao kwa kuwa nawafahamu wote waliohusika katika
tukio hilo ….. nawafahamu wanafunzi wake wa kidato cha sita ila
wale wa kidato cha tano sikuweza kuwatambua kwa kuwa wamejiunga
na shule hii hivi karibuni …..
Ukweli ni kwamba sikotayari kabisa i kukanyaga tena kwenye
shule hiyo kwani maisha yangu yako hatarini hivyo naomba
nitafutiwe shule nyingine ya kufundisha na ikiwezekana iwe
nje ya mkoa Katavi ‘alisisitiza .
Kabla ya tukio hilo Mwalimu Makonda Ng-oga alifikishwa katika
Mahakama ya Wilaya ya Mpanda hapo Aprlii 28 mwaka huu na
kusomewa mashitaka ya tuhuma za kulawiti mwanafunzi wake wa
kiume wa kidato cha sita kwa vipindi tofauti vya kuanzia
Novemba mwaka jana hadi Aprii mwaka huu.
Nae Mwalimu Gabriel Kambona alidai kuwa yeye hayuko tayari
kuendelea kufundisha kwenye shule hiyo kwamba kitendo cha kupigwa
na wanafunzi wake kimemfedhesha .
.Kwa mujibu wa mwalimu huyo walimu wa shule hiyo waliketi baada ya
kutokea kwa tukio hilo ambapo walifikia maamuzi kuwa wanafunzi wote
waliobinika kushiriki kuwashamulia walimu wao wasimamishe shule
akidai kuwa uongozi wa Halmashauri ya Mpimbwe na wilaya ya Mlele
ulipiga .
“Nimesikitishwa sana na majibu yaliyotolewa na viongozi wa
wilaya ya Mlele walipohoji nimejiingizaje mpaka nikapingwa na
wanafunzi kama alivyopigwa mwalimu Makonda majibu haya
nidhahri kuwa wanalidhika na sisi kupigwa na wanafunzi wetu …..
Nimeandika barua ya kuomba uhamisho kwani nia aibu kwangu
kuendelea kufundisha wanafunzi ambao wamenishambukia na kunitoa
ngeo kichwani ….. siku hiyo ya tukio niliibiwa simu mbili za
kiganjani lakini jana nimefanikiwa kuikamata simu moja kwa
mwanafunzi wa kidato cha tano anayeitwa , Alex Maiko Makona
na tayari amemfikisha katika Kituo cha Polisi cha Usevya”
alisisitiza .
Kwa upande wake , Mwenyekiti wa Chama cha Walimu (CWT) Mkoa wa
Katavi, Gregori Mshota alikiri kufahamu mkasa huo wa
kushambuliwa na kujeruhiwa kwa waili wawili katika Shule ya
Sekondari Usevya ambapo mmoja wao alilazwa katika Hospitali ya
Manispaa ya Mpanda kwa matibabu ..
“ Chama (CWT) hicho tayari kimeanza kuwsiliana na uongozi
wa Halmashauri ya Mpimbwe na uongozi wa Wilaya ya Mlele
ili kuhakikisha mwalimu huyo anakuwa salama ……
Kwa sasa jambo hili halihitaji mjadala zaidi kinachotakiwa
ni mwalimu huyo kupangiwa kituo kingine cha kazi ili
kununusuru uhai wakwe uamuzi huu ulipaswa uwe umefanyika
mapema “ alisisitiza .
Nae Ofisa Elimu wa Mkoa wa Katavi , Ernesti Hinju
alipotafutwa ili aweze kuelezea tatizo hilo alisema yeye yuko
nje ya mkoa kikazi ila swala hilo lipo katika ofisi
yake na wameisha anza kulichakata .
Alisema swala hilo linahitaji vyombo mbalimbali kwa ajiri ya
kulipatia ufumbuzi swala hilo ikiwemo bodi ya shule ya
Sekondari ya Usevya .
Wakati wa ziara ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alioifanya
mwezi uliopita mke wa Mwalimu Makonda Ng-oga alikwenda
kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kijiji cha Maji
Moto huku akiwa na bango la lililokuwa limeandikwa juu ya
familia yake kutishiwa amani hari ambayo ilimfanya Waziri
Mkuu amwagize Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi
ashughulikie swala la malalamiko hayo .
Juhudi za kumpata aliyekuwa mwanafunzi wa shule hiyo
aliyemaliza kidato cha sita mwaka huu ambae anatuhumiwa
kulawitiwa na mwalimu huyo aliaweze kuthibitisha mahusiano yake
na Makonda azikuweza kufanikiwa hakuweza kupatikana kwa njia
ya simu huko aliko Wilayani Misungwi.
Mwisho
‘(34)ambaye amengolewa meno yake matano .
Inadaiwa kuwa wanafunzi wa kidato cha sita shuleni hapo hawamtaki
Makamu Mkuu wa Shule hiyo kuendelea kufundisha shuleni hapo
kutokana kile wanacho dai kuwa na tabia yake ya kuwadhalilisha wanafunzi wa kiume
shuleni hapo.
Mwezi Mei mwaka huu Ng’oka “Membele” amefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Mpanda kwa tuhuma za kumlawiti mwanafunzi wake kidaiwa kutenda
kosa hilo kati ya Novemba 2015 na April mwaka huu
Inadaiwa kuwa kukamatwa na kufikishwa mahakamani kwa Makamu Mkuu huyo
wa shule hiyo kulifuatia wanafunzi wa kiume wanaosoma Kidato cha Tano
sasa wako Kidato cha Sita katika shule hiyo kumkataa na kutishia
kuandamana kupinga vitendo vyake vya kuwalawiti wanafunzi wake.
Wanafunzi hao walidai kuwa mwalimu huyo amekuwa akiwalawiti baadhi yao
ikiwa ni adhabu mbadala wanapobainika kufanya makosa shuleni hapo.
Hata hivyo baada ya kutopatikana ushahidi wa kumtia hatiani
Mwalimu Makonda ambapo Julai 27 mwaka huu Mahakama ya Hakimu
Mkazi ya Wilaya ya Mpanda ilimwachia huru .
Inadaiwa kuwa baada ya mahakama hiyo kumwachia huru Mwalimu
Makonda aliripoti kwenye kituo chake cha kazi , Shule ya
Sekondari Usevya , Agosti Mosi mwaka huu ambapo kurejea kwake
shuleni hapo kunadaiwa kuamsha hasira kwa wanafunzi wa Kidato cha
Sita wakidai hawapo tayari kumwona mwalimu huyo na familia yake
shuleni hapo .
Akiongea na wanahabari jana mjini hapa Ng’oka alidai kuwa hayuko
tayari kuendelea kufundisha kwenye shule hiyo kwa kuhofia
usalama wake kutoka na kipigo alichokipata cha kushambuliwa na
baadhi ya wanafunzi wake wa kidato cha tano na cha sita wakati
akiwa nyumbani kwake na familia yake .
Akisimulia mkasa huo alisema siku hiyo ya tukio , Agosti 12
mwaka huu alikuwa nyumbani kwake shuleni hapo pamoja na
familia yake pamoja na mwalimu mwenzake aitwae, Gabriel
Kambona aliyekuwa amemtembelea ..
“ Ghafla, saa mbili usiku nikiwa maliwatoni nikioga lilitokea
kundi la wanafunzi wa kidato cha tano na sita wakiwa na silaha za
jadi kama vile fimbo , malungu , mawe na matofali na kuanza
kuishambulia familia yake pamoja na mwalimu Kambona” alieleza
Alidai kuwa alilazimika ‘kuchomoka’ bafuni baada ya kusikia mayowe
yaliyokuwa yakipigwa na familia yake wakiomba msaada ambapo
alipofika sebuleni alishuhudia wanafunzi hao wakiishamulia familia
yake .
“Ndipo walinigeukia na kuanza kunishamubulia kwa kunipiga kwa
marungu na fimbo hadi nikapoteza fahamu nilizinduka nikiwa
nimelazwa kwenye Kituo cha Afya Usevya na kubaini kuwa nimepoteza
meno yangu matano huku nikiwa nimejeruhiwa kichwani ….
. baadae nilihamishiwa katika Hospitali ya Wilaya ya Mpanda
ambako nililazwa wiki moja na nusu kwa matibabu na sasa nimepewa
rufaa niende Hospitali ya Taifa Muhimbili Jijini Dar kwa matibabu
zaidi” alieleza
Alidai kuwa uhasama baina yake na wanafunzi hao umedumu kwa
muda mrefu lakini anashangaa uongozi wa Halmashauri ya Mpimbwe
na Wilaya ya Mlele umeshindwa kumpangia kituo kingine cha
kazi .
“Isitoshe uongozi wa Halmashauri ya Mpimbwe na wa wilaya ya
Mlele haujawachukulia hatu yeyote wanafunzi hao licha ya
kupeleka majina yao kwa kuwa nawafahamu wote waliohusika katika
tukio hilo ….. nawafahamu wanafunzi wake wa kidato cha sita ila
wale wa kidato cha tano sikuweza kuwatambua kwa kuwa wamejiunga
na shule hii hivi karibuni …..
Ukweli ni kwamba sikotayari kabisa i kukanyaga tena kwenye
shule hiyo kwani maisha yangu yako hatarini hivyo naomba
nitafutiwe shule nyingine ya kufundisha na ikiwezekana iwe
nje ya mkoa Katavi ‘alisisitiza .
Mahakama ya Wilaya ya Mpanda hapo Aprlii 28 mwaka huu na
kusomewa mashitaka ya tuhuma za kulawiti mwanafunzi wake wa
kiume wa kidato cha sita kwa vipindi tofauti vya kuanzia
Novemba mwaka jana hadi Aprii mwaka huu.
Nae Mwalimu Gabriel Kambona alidai kuwa yeye hayuko tayari
kuendelea kufundisha kwenye shule hiyo kwamba kitendo cha kupigwa
na wanafunzi wake kimemfedhesha .
.Kwa mujibu wa mwalimu huyo walimu wa shule hiyo waliketi baada ya
kutokea kwa tukio hilo ambapo walifikia maamuzi kuwa wanafunzi wote
waliobinika kushiriki kuwashamulia walimu wao wasimamishe shule
akidai kuwa uongozi wa Halmashauri ya Mpimbwe na wilaya ya Mlele
ulipiga .
“Nimesikitishwa sana na majibu yaliyotolewa na viongozi wa
wilaya ya Mlele walipohoji nimejiingizaje mpaka nikapingwa na
wanafunzi kama alivyopigwa mwalimu Makonda majibu haya
nidhahri kuwa wanalidhika na sisi kupigwa na wanafunzi wetu …..
Nimeandika barua ya kuomba uhamisho kwani nia aibu kwangu
kuendelea kufundisha wanafunzi ambao wamenishambukia na kunitoa
ngeo kichwani ….. siku hiyo ya tukio niliibiwa simu mbili za
kiganjani lakini jana nimefanikiwa kuikamata simu moja kwa
mwanafunzi wa kidato cha tano anayeitwa , Alex Maiko Makona
na tayari amemfikisha katika Kituo cha Polisi cha Usevya”
alisisitiza .
Kwa upande wake , Mwenyekiti wa Chama cha Walimu (CWT) Mkoa wa
Katavi, Gregori Mshota alikiri kufahamu mkasa huo wa
kushambuliwa na kujeruhiwa kwa waili wawili katika Shule ya
Sekondari Usevya ambapo mmoja wao alilazwa katika Hospitali ya
Manispaa ya Mpanda kwa matibabu ..
“ Chama (CWT) hicho tayari kimeanza kuwsiliana na uongozi
wa Halmashauri ya Mpimbwe na uongozi wa Wilaya ya Mlele
ili kuhakikisha mwalimu huyo anakuwa salama ……
Kwa sasa jambo hili halihitaji mjadala zaidi kinachotakiwa
ni mwalimu huyo kupangiwa kituo kingine cha kazi ili
kununusuru uhai wakwe uamuzi huu ulipaswa uwe umefanyika
mapema “ alisisitiza .
Nae Ofisa Elimu wa Mkoa wa Katavi , Ernesti Hinju
alipotafutwa ili aweze kuelezea tatizo hilo alisema yeye yuko
nje ya mkoa kikazi ila swala hilo lipo katika ofisi
yake na wameisha anza kulichakata .
Alisema swala hilo linahitaji vyombo mbalimbali kwa ajiri ya
kulipatia ufumbuzi swala hilo ikiwemo bodi ya shule ya
Sekondari ya Usevya .
Wakati wa ziara ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alioifanya
mwezi uliopita mke wa Mwalimu Makonda Ng-oga alikwenda
kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kijiji cha Maji
Moto huku akiwa na bango la lililokuwa limeandikwa juu ya
familia yake kutishiwa amani hari ambayo ilimfanya Waziri
Mkuu amwagize Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi
ashughulikie swala la malalamiko hayo .
Juhudi za kumpata aliyekuwa mwanafunzi wa shule hiyo
aliyemaliza kidato cha sita mwaka huu ambae anatuhumiwa
kulawitiwa na mwalimu huyo aliaweze kuthibitisha mahusiano yake
na Makonda azikuweza kufanikiwa hakuweza kupatikana kwa njia
ya simu huko aliko Wilayani Misungwi.
Mwisho
0 comments:
Post a Comment