Home » » MAJALIWA KUANZA ZIARA YA SIKU NNE KATAVI

MAJALIWA KUANZA ZIARA YA SIKU NNE KATAVI


      Na  Walter   Mguluchuma     Katavi.
WazirI  Mkuu  wa  Jamuhuri  ya Muungano wa Tanzania  Kassimu Majaliwa  anatarajiwa kuanza  kufanya ziara ya siku nne  Mkoani  Katavi  ambapo atatembelea na kukagua  miradi  mbalimbli ya maendeleo pamoja na kuzungumza na  Wananchi  kwenye Mikutano ya  hadhara itakayofanyika  katika  Halmashauri zote za  Mkoa wa Katavi .
Kwa  mujibu wa ratiba iliyotolewa kwa vyombo vya  Habari na  Katibu  Tawala  Msaidizi wa  Mkoa wa  Katavi  Lautel   Kanoni  ziara  hiyo ya Waziri Mkuu Majaliwa   inatarajiwa kuanza leo  Agosti  20   hadi  Agosti  23 .
Kwa  mujibu wa  ratiba   hiyo Waziri Mkuu atawasili   katika  uwanja wa  Ndege wa  Mpanda leo  mchana   kwa ndege na kisha   ataelekea  Ikulu  Ndogo ya  Mpanda  ambapo  atasomewa  taarifa ya  Mkoa na kisha atazungumza na  watumishi wa  Serikali  katika  viwanja vya Ikulu  ndogo ya  Mpanda.
Siku  itakayofuata  atakwenda  katika Kijiji cha  Majalila  kwa ajili  ya kuona  eneo  zitakapojengwa Ofisi   za  Halmashauri ya Wilaya ya  Mpanda  na kutembelea  mradi wa maji  katika  Kijiji  hicho  na kisha atawahutubia wananchi   kwenye  mkutano  wa  hadhara.

Siku  hiyo  pia  atawahutubia   Wananchi  katika   mikutano ya  hadhara  itakayofanyika  katika   eneo  la Kijiji cha  Ndui  Makazi ya wakimbizi ya  Katumba na   katika    uwanja wa  Azimio   Mjini  Mpanda .
Agsti  22 Waziri  Mkuu atafanya  ziara ya siku  moja  katika   Wilaya ya  Mlele   ambapo  atawahutubia  wananchi wa Inyonga katika  Halmashauri ya Wilaya ya  Mlele na    na  baadaye elekea  katika  Kijiji cha  Majimoto Halmashari ya  Mpimbwe na   atakagua ujenzi wa   Daraja  la mto Kavuu na kisha    atawahutubia wananchi wa Kijiji  hicho katika   mkutano wa  Hadhara.
 Waziri  Mkuu  Majaliwa  Agosti 23 atafanya mkutano wa majumuisho ya ziara yake katika   ukumbi wa   Idara ya   Maji   Mjini  hapa  na    ataelekea   Wilayani  Nkasi Mkoa wa  Rukwa .
 Baada  ya  ziara  yake   Mkoani  Rukwa  Majaliwa  siku ya tarehe  26 atakwenda   Kijijini kwake   Mizengo  Kijiji  cha      Kibaoni  Wilayani  Mlele  Mkoa wa  Katavi  ambapo  atafanya  mazungumzo na  Waziri  Mkuu Mstaafu  Mizengo  Pinda na  kasha  atatembelea  shule  ya  Msingi ya  Kakuni aliyosoma  Pinda  na siku hiyo hiyo  ataondoka kwa ndege  katika  uwanja wa ndege wa Mpanda ikiwa  ndio mwisho wa ziara yake ya mikoa ya  Katavi na  Rukwa .

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa