Home » » MWANAFUNZI WA MIAKA 12 AFA MAJI MTONI WAKATI AKIWA ANAVUA SAMAKI

MWANAFUNZI WA MIAKA 12 AFA MAJI MTONI WAKATI AKIWA ANAVUA SAMAKI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

 Kamanda wa Polisi Mkowa wa Katavi Dhahiri Kidavashari
MWANAFUNZI AFA MAJI MTONI WAKATI AKIWA  ANAVUA SAMAKI
Na  Walter Mguluchuma
Katavi yetu blog
Mwanafunzi wa darasa la sita  shule ya Msingi Kashato Manspaa ya Mpanda Julias  Justine 12  amekufa maji  wakati akiwa anavua samaki  katika mto Mpanda  eneo la Kigamboni  wakati akiwa na wanafunzi wenzake.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi Dhahiri Kidavashari aliwaambia jana waandishi wa habari  jana  kuwa tukio hilo lilitokea hapo juzi  majira ya saa saa sita mchana katika  mto Mpanda eneo la Kigamboni.
Siku hiyo  ya tukio mama  mzazi  wa marehemu  anaitwa Prisca  Selemani  alimwagiza  marehemu dukani  kwenda kununua sabuni ya kufulia nguo baada ya kuwa amemwagiza  yeye alikwenda  msibani katika Mtaa wa Nsemlwa.

Kamanda Kidavashari alieleza  wakati marehemu alipokuwa anakwenda dukani alikutana na watoto wenzake ambao walimshawishi asiende kununua sabuni na badala yake wakanunue doano ya kuvulia samaki  nae alikubaliana na watoto wenzake  na alinunua doano badala ya sabuni na kasha walielekea mtoni kuvua samaki.
Mama yake  yake  alirudi nyumbani  muda wa saa 12 jioni  kutoka msibani alikokuwa amekwenda  na hakuweza  kumkuta nyumbani  na alianza kumkutafuta  kwa majirani zake  na kuweza kufanikiwa kumpata.
Alisema  ndipo hapo jana  walipomweleza kuwa walimwona  mwanae akiwa anavua samaki  kwenye mto wa Mpanda  eneo la Kigamboni  huku akiwa na watoto wenzake.
Ndipo jitihada za kumtafuta  zilipoanza  za  kwenye mto Mpanda  na ilipofikia majira ya saa nne asubuhi  walipofanikiwa  kuupata mwili wa marehemu akiwa ameisha kufa maji katika mto eneo la Kigamboni.
Kidavashari alisema baada ya mwili wa marehemu kufanyiwa uchunguzi walikabidhiwa ndugu wa marehemu kwa ajiri ya mazishi ambapo mazishi yalifanyika katika  makaburi ya Shanwe.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi ametowa wito  kwa jamii kuwaelimisha watoto kuacha tabia  ya kwenda  kucheza ,kuogelea au kuvua samaki  kwenye mito na madimbwi hasa wakati huu wa mvua  ili kuweza  kujiepusha  na matukio ya namna hii yasijitokeze ndani ya jamii

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa