Na Walter
Mguluchuma
Katavi
Mnyama Simba
amevamia Kijiji cha Sitalike Tarafa ya
Nsimbo Wilaya ya Mlele Mkoa wa Katavi na kuuwa watu wawili mtu na mtoto wake
kwa kumla mtoto na kuachi kichwa na baba yake mzazi kunyonywa damu na simba huyo hadi kufariki
Dunia.
Tukio la Simba huyo kuuwa watu wawili
limetokea hapo hapo jana majira ya saa kumi na moja alifajiri katika Kijiji
hicho cha Sitalike .
Mwenyekiti wa
Kijiji hicho Cristophar Anjelo aliwaambia waandishi wa Habari jana kuwa
marehemu waliouwawa na Simba
kuwa ni John Jeremia (45) na mwanae wa kiume mwenye umri wa miaka mitano .
Alisema
siku hiyo ya tukio wanafamilia hao walikuwa wamelala ndani ya nyumba
yao ndipo simba huyo jike alipovamia na
kuingia ndani ya nyumba hiyo ambayo haikuwa na uwimala na kuwavaa watu mtu na mtoto wake .
Alieleza
baada ya Simba huyo kuingia ndani alimvamia baba wa mtoto huyo na kuanza kumnyonya damu hadi alipohakikisha amefariki
Dunia ndipo alipo mwachia marehemu huyo.
Mwenyekiti huyo
wa Kijiji alisema simba huyo baada ya
kuona John Jeremia amemnyonya damu hadi kufa alihamia
kwa mtoto wake na marehemu na kuanza
kumshambulia na kisha alianza kumtafuna
na kubakia kichwa huku mwili wake wote wa mtoto huyo kuliwa wote.
Simba
baada ya kuwa amekula mwili wa mtoto alichukua kichwa cha marehemu mtoto
na kwenda nacho hadi kwenye kichaka
kilichokuwa jirani na nyumba ya marehemu hao.
Alisema taarifa za kuuwa na simba kwa marehemu
hao zilifika kwenye uongozi wa Kijiji hicho ambao nao walitowa taarifa kwa
Askari wa Hifadhi ya Taifa ya Katavi ambapo walianza kufanya msako wa kumsaka
simba huyo kwa kushirikiana na Wananchi wa Kijiji cha Sitalike.
Wakati walipokuwa wakifanya msako walionanyayo
za simba na walizifuata kule
zilipoelekea na walipofika kwenye kichaka walimuona simba huyo akiwa amekaa na
pembeni yake kukiwa na kichwa cha
marehemu mtoto .
Mwenyekiti wa
Kijiji alisema Askari wa Hifadhi ya
Katavi walimfyatulia simba huyo risasi lakini aliweza kuikwepa na kusogea mbele zaidi .
Hata hivyo
waliendelea kumfuata kwa kushirikiana na
wananchi ndipo Askari wa TANAPA walipofanikiwa
kupiga risasi na kufa hapo hapo
Alieleza baada ya
Simba huyo kuwa ameuwawa kwa kupigwa
risasi baadhi ya wananchi waliomba wamchukue
kama kitoweo cha mboga lakini
Askari wa TANAPA waliwakatalia na walimchukua simba huyo aliyekuwa amekufa na kwenda
nae kwenye hifadhi yao kwa kile
walichoeleza kuwa wanakwenda kumchoma moto kwa kutumia mafuta ya petroli.
Kamanda wa Polisi
wa Mkoa wa Katavi Dhahiri Kidavashari amethibitisha kuuwawa kwa watu hao na
Simba huyo aliyetokea kwenye Hifadhi ya mbuga ya Katavi .
Alisema ameisha peleka askari wake kwenda
kuangalia eneo la tukio hilo na ametowa
wito kwa wananchi kuacha kujenga makazi karibu na hifadhi ya Katavi
0 comments:
Post a Comment