Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Na Walter Mguluchuma
Katavi
. JESHI la polisi mkoa wa Katavi limegoma kuusafirisha mwili wa askari
polisi PC H 305 Nobart Chacha(25) ambaye aliuawa kwa kupigwa risasi
kifuani wakati akifanya ujambazi nyumbani kwa mfanyabiashara mmoja wa
madini.
Kwa mujibu wa habari zilipatikana kutoka mjini Mpanda, zinaeleza kuwa
mwili wa marehermu huyo umesafirishwa jana kuelekea mkoani Mara ambapo
baadhi ya marafiki,Chama cha watu wa Mara waishio mkoani Katavi ndio
walichukua jukumu la kugharamia usafirishaji wa mwili huo.
MMoja wa wajumbe katika Chama hicho, Julius Marwa alisema kuwa
wamelazimika kusafirisha mwili huo wa marehemu baada ya polisi kukataa
kuusafirisha kwa madai kwa kitendo alichofanya askari huo tayari
amejifukuzisha kazi.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Katavi, Dhahiri Kidavashari alisema kwamba kwa
taratibu za kijeshi mwili wake haustahili pewa heshima yoyote ikiwa
pamoja na kusafirishwa kwa kuwa tayari amejifukuzisha kwa aibu na fedhea
kubwa kutokana na kitendo alichofanya.
Askari Polisi huyo wa kituo cha polisi wilaya ya Mpanda, aliuawa majuzi
nyakati za usiku wakati akiwa katika harakati za kufanya ujambazi
nyumbani kwa mfanyabiashara wa madini Daniel John katika Kijiji cha
Ibindi kilichopo Kata ya Machimboni Wilayani Mlele.
Kwa mujibu wa Diwani wa Kata ya Machimboni, Raphael Kalinga, polisi
huyo akiwa na kundi la majambazi wenzake ambao idadi yao hakufahamika
mara moja walifika kijijini hapo kwa lengo la kumvumia na kumpora kwa
kutumia silaha mfanya biashara huyo wa Madini ya dhahabu na mashine za
kusaga.
Inadaiwa kuwa, majambazi hao walivunja mlango kuingia ndani ya nyumba
hiyo na kumwamuru mfanyabiashara huyo kukaa kimya lakini hakutii agizo
hilo ambapo alichukua bunduki yake ya aina ya Shortgun na kufyatua
risasi ambayo ilimpiga Askari Polisi huyo katika sehemu ya kifuani na
mgongoni na kufa hapo hapo.
Home »
» JESHI la polisi mkoa wa Katavi limegoma kuusafirisha mwili wa askari polisi PC H 305 Nobart Chacha(25) ambaye aliuawa kwa kupigwa risasi kifuani wakati akifanya ujambazi
0 comments:
Post a Comment