Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Na Walter Mguluchuma
Katavi yetu blog
Askari wa Jeshi la Polisi wa Wilaya ya Mpanda Mkoa Katavi Pc H 305 Nobart Chacha(25) ameuwawa kwa kupigwa Risasi kifuani na mgongoni wakati akiwa anataka kufanya ujambazi na kupora mali za mfanyabiashara wa Madini.
Mauwaji ya Askari wa huyo wa jeshi la Polisi lilitokea hapo jana muda wa saa nane usiku katika Kijiji cha Ibindi Kata ya Machimboni Wilayani Mlele.
Diwani wa Kata ya Machimboni Raphael Kalinga aliwaambia Waandishi wa Habari kuwa Askari
Polisi huyo akiwa na kundi la majambazi wenzake ambao idadi yao
hakufahamika walifika kijijini hapo kwa lengo la kumvumia na kumpora kwa
kutumia mapanga na shoka mfanya biashara wa Madini ya dhahabu na mashine za kusaga aitwaye Daniel John.
Alisema baada ya kuwa wamefika nyumbani kwa mfanyabiashara huyo walivunja mlango wa mbele wa nyumba ya mfanya biashara huyo ambae alikuwa amelala ndani ya chumba chake .
Majambazi hao baada ya kuvunja mlango waliingia ndani na mfanya biashara huyo aliwauliza kuwa wao ni akinanani na ndipo walipomwamuru kuwa asipige kelele na anyamaze kimya vinginevyo watamuuwa.
Diwani Kalinga ambae ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimmbo alieleza ndipo Daniel John
alipojiandaa na kuchukua bunduki yake ya Shorti gani na kufyatua risasi
ambayo ilimpiga Askari Polisi huyo katika sehemu ya kifuani na mgongoni
na kufa hapo hapo .
Alisema
majambazi wenzake ambao walikuwa na silaha za jadi baada ya kuona
mwenzao kapigwa risasi na kufa waliamua kumbeba marehemu na kwenda
kumtupa kichani umbali wa mita 200 kutoka kwenye eneo la tukio na kisha
walitokomea kusiko julikana.
Wakazi wa Kijiji hicho walifika nyumbani kwa mfanyabiashara huyo na kukuta michirizi ya damu na ndipo walipoamua kuifuata iliko kuwa inaelekea.
Alisema wanakijiji waliendelea kuifuata michirizi ya damu na ndipo walipofika umbali wa mita 200 kutokea nyumbani kwa Daniel John waliweza kuuwona mwili wa Askari Polisi ambae alikuwa tayari amefariki Dunia na ndipo taarifa zilipotolewa kwa jeshi la polisi Wilaya ya Mpanda.
Polisi walifika kwenye eneo hilo baada ya muda mfupi na ndipo walipoweza kumtambua marehemu kuwa ni Askari polisi wa kituo cha polisi cha Wilaya ya Mpanda .
Kamanda
wa Polisi wa Mkoa wa Katavi Dhahiri Kidavashari amethibitisha kutokea
kwa tukio la askari huyo kuuwawa kwa kupigwa risasi wakati akiwa anataka
kufanya ujambazi na kupora .
Alisema mwili wa marehemu bado umehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti katika Hospitali ya Wilaya ya Mpanda .
Kabla ya tukio hilo kulikuwa na malalamiko kutoka
kwa wananchi wa Mkoa wa Katavi waliokuwa wakiwatuhumu baadhi ya askari
wa Jeshi la polisi kuhusika katika matukio mbalimbali yaliyakuwa
yakitokea ya ujambazi na uporaji katika maeneo ya Mkoa wa Katavi.
0 comments:
Post a Comment