Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Na Walter
Mguluchuma
Katavi
Mkazi wa Mtaa wa Mapinduzi Kata ya Ilembo Wilaya ya Mpanda Omari Salehe(35) amefariki Dunia baada ya
kunywa pombe nyingi kupita kiasi bila kura chakula
Kwa mujibu wa
majirani wa marehemu huyo ambao
hawakutaka majina yao kutajwa
gazetini walisema kuwa marehemu huyo alifariki Dunia hapo
jana majira ya saa sita mchana
nyumbani kwake katika Mtaa wa
Mapinduzi
Walisema kuwa siku moja kabla ya kifo
hicho marehemu alishinda kutwa nzima kwenye klabu
kinachouza pombe ya kienyeji aina ya
komoni
Siku hiyo
baada ya kunywa pombe nyingi
kupita kiasi bila kura alijikuta
ameshindwa kuingia ndani ya nyumba yake ambayo alikuwa akiishi peke yake na
badala yake alilala
nje ya nyumba yake hadi
ambapo aliamushwa na majirani zake walipita jirani na nyumba yake siku iliyofuata majira ya
saa moja asubuhi
Baada ya marehemu kuamshwa na majirani
zake aliingia ndani ya
nyumba yake na kisha alitoka na kuelekea katika ofisi
ya Mtendaji wa Mtaa
kusikiliza shauri lale la kuhusiana na mgogoro wa kiwanja huku akiwa ajakula chakula chochote
Walieleza mara baada ya kutoka kwenye shauri hilo
majira ya saa tatu asubuhi
alielekea moja kwa moja kwenye
klabu ya pombe na kuendelea kunywa
huku akiwa ajakula chakula chochote
Marehemu baada ya
kuona amezidiwa na pombe alizokuwa
amekunywa aliamua kurudi
nyumbani kwake na kuingia ndani na kukaa kwenye kiti na baada ya muda
mfupi akafariki Dunia
Marehemu Omari
Salehe amezikwa jana kwenye makabuli ya
Mwanasega Kata ya Ilembo Wilayani hapa
na kifo hicho kimeleta huzuni kubwa kwa wananchi wa Mtaa huo
Home »
» AFA BAADA YA KUNYWA POMBE NYINGI KUPITA KIASI BILA KULA CHAKULA
0 comments:
Post a Comment