Home » » HOOOOT: MGOMBEA UBUNGE KUTUMIA MSHAHARA WAKE KUBORESHAFYA YA MAMA NA MTOTO MCHANGA

HOOOOT: MGOMBEA UBUNGE KUTUMIA MSHAHARA WAKE KUBORESHAFYA YA MAMA NA MTOTO MCHANGA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Na  Walter  Mguluchuma
Katavi
Mgombea wa  Ubunge wa Jimbo la  Kavuu Mkoani  Katavi kupitia    CHADEMA  Laulent  Mangweshi  ameahidi kuwa endapo atachaguliwa kuwa Mbunge wa Jimbo la Kavuu atahakikisha  anatowa nusu ya  fedha za mshahara  wake zitumike  kwa ajiri ya kuokoa kuokoa  uhai mama na mtoto
Mgombe huyo alitowa kauli hiyo  hapo jana wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari  katika  Kijiji cha Majimoto  Wilayani  Mlele
Mgombea ubunge huyo alisema  wanawake wangi na watoto  wachanga wanapoteza maisha  kutokana  na  ukosefu wa huma za afya kuwa mbali na wanako ishi
 Alisema  kutokana na hari hiyo  ndio maana kwenye  mikutano yake ya kampeni za kugombea ubunge wa jimbo la Kavuu swala la uhai wa mama na mtoto amelipa kipaumbele  cha kwanza  na hata kwenye mabango yake ya kampeni ndio maana ameandika atahakikisha ana ukoa vifo vya mama na mtoto mchanga
Alifafanua kuwa   endapo atachaguliwa kuwa Mbunge wa Jimbo hilo  atatowa  nusu ya fedha za mshahara wake zitumike kwa ajiri ya shughuli za kuokoa uhai wa mama na mtoto mchanga  na  pia atahakikisha ananunua gari  kwa  ajiri ya  wajawazito na watoto wachanga
Alisema  kwenye jimbo lake  ataakikisha akina baba na akina  mama  wana wanapatiwa elimu ya uzazi wa mpango kabla hawaja anza kutumia dawa za uzazi wa mpango  kwani wapo baadhi ya akina mama wamekuwa wakipewa dawa za uzazi wa mpango na wamekuwa hawazitumii kwa ajili ya kukosa elimu
Mangweshi  alieleza kuwa atajitahidi kuondoa tatizo la wasichana  kupata mimba wakiwa na umri mdogo kwa kuishauri Wizara ya Elimu  kujenga  mambweni kwenye shule zote za kata kwa wanafunzi wakike  itakuwa kwake ni mwiko kuishi kwenye nyumba za kupanga jijijini  ambako wanaishi bila uangalizi wa wazazi na waalimu
Nae  mgombea wa ubunge wa jimbo la Kavuu kupitia  chama cha ACT  Wazalendo Tanzania Sintansilau  Kisesa yeye ameleza kuwa endapo atachaguliwa kuwa  mbunge wa jimbo hilo  ataakikisha vituo vya afya na zahanati zinaimalishwa ili  akina mama na watoto wewe wanapatiwa  huduma bora zitakazo wawezesha kuokoa uhai wao
Pia ataishauri Serikali na Halmashauri yake itenge   bajeti ya    Afya ya  kutosha ili  kusiwepo na tatizo la  upungufu wa dawa  na  vifaa kwenye  vituo vya afya na zahanati kwenye jimbo lake
 Alisema  ataweka  utaratibu wa  kutolewa kwa kwa elimu ya uzazi wa mpango   kwenye jimbo lake  kwa njia ya  sinema     na vipeperushi
Na atahakikisha  kwenye vituo vya afya huduma ya upasuaji   inatplewa kuliko ilivyo sasa ambapo huduma hiyo ya upasuaji inatolewa katika Hospitali ya Wilaya ya Mpanda hali ambayo imekuwa ikisababisha wanawake kupoteza maisha kwa kuchelewa kufika  Hostalini kutona na umbali
Pia  ataishauri Serikali ipige marufu wasichana wote wenye umri wa chini ya miaka 19 kuingia kwenye nyumba za kulala wageni kwani zimekuwa zikichangia wasichana kupata mimba  zembe

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa