Home » » HOT NEWS: WALIOKUWA RAIA WA BURUNDI WANAISHI KWENYE MAKAZI YA WAKIMBIZI YA KATUMBA NA MISHAMO WAHAIDI KUMPA KURA DK JOHN MAGUFULI

HOT NEWS: WALIOKUWA RAIA WA BURUNDI WANAISHI KWENYE MAKAZI YA WAKIMBIZI YA KATUMBA NA MISHAMO WAHAIDI KUMPA KURA DK JOHN MAGUFULI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Na  Walter  Mguluchuma
Katavi yetu Blog
 Wananchi  waliokuwa  Raia wa  Nchi ya Burundi  ambao wamepewa Uraia na Serikali ya Tanzania  hivi  karibuni  wanaishi  katika  Makazi ya Katumba na Mishamo Mkoani  Katavi wamehaidi  kupigia  kura  mgombea wa Urais(CCM) Dk  John  Magufuli wakati wa uchaguzi mkuu wa oktoba 25
Raia  hao wapi  walitowa   ahadi  hiyo kwa  wakati  fofauti   hapo jana  kwenye  mikutano  ya  hadhara ilifanyika kwenye kijiji cha  Kanoge makazi ya wakimbizi ya Katumba  na Mishamo  wakati walipokuwa wakitutubiwa  na mgombea  Urais(CCM)
 Wananchi  walimweleza  mgombea   huyo  kuwa  wanatambua  na kuthamini  jitihada  zilizofanywa  na CCM  hadi  wakakubaliwa kupewa  uraia  Watanzania
 Katika hotuba yake Magufuli  aliwaeleza  Wananchi  hao kuwa  Serikali ya  Tanzania imewapatia Uraia  hivyo watambue kuwa maisha yao yote  kwa sasa yatakuwa Tanzania
Hivyo  wanatakiwa kufanya kazi kwa bidii   ilikujiletea  maendeleo yao na  Nchi kwa ujumla  na  endapo atachaguliwa kuwa Rais wa awamu ya tano serikali yake itawatatulia  kero  walizo nazo
Kwa upande  Mjumbe wa Kamati ya CCM  ambae pia Waziri  Mkuu  Mizengo  Pinda  alieleza kwenye mikutano  hiyo ya  hadhara kuwa  Serikali ya CCM ilikubali kuwapatia Urai wa Tanzania  waliokuwa Raia wa Burundi ambao kwa hiyari yao wenyewe waliomba kuwa Raia wa Tanzania
Katika   zoezi lililofanyika  hivi  karibuni   walikuwa Raia wa Burundi 112,000 walikuwa wakiishi kwenye  makazi ya wakimbizi ya Katumba na Mishamo  Mkoani  Katavi walipewa vyeti vya uraia wa Tanzania

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa