Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Na Walter
Mguluchuma
Katavi
Watu sita wakazi wa Kijiji cha
Ikola Wilaya ya Mpanda
Mkoa wa Katavi wanashikiliwa
na jeshi la Polisi
kwa tuhuma za kuvamia kituo
cha Polisi cha Ikola
na kutaka kukichoma moto huku wakiwa na silaha za jadi baada
ya kukasilishwa na kitendo cha
Mwenyekiti wao wa kitongoji cha Mpalamawe B kukataa kuwatambua watu
waliotajwa majina yao kwenye
mkutano wa hadhara kuwa ni wachawi (washirikina)
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi aliwaambia waandishi wa habari
jana kuwa tukio
hilo lilitokea hapo
juzi majira ya saa kumi jioni Kijijini
hapo
Aliwaja watuhumiwa wanao shikiliwa na
jeshi la Polisi kuwa ni
Pascal Dominiki( 30, Mirambo Kasimu
wa Kijiji cha Ikola
Wilaya ya Mpanda
Nikwamba
siku moja ya tukio hilo
kilifanyika kikao cha
Baraza la wazee wa Kitongoji cha
Mpalamawe B kilichohusishwa na
imani za ushirikina wa kujadili vifo vya watu ambavyo vimekuwa
vikitokea hivi karibuni
na katika kikao
hicho mwenyekiti wao
wakitongoji Hilali Rashid
alikuwa ni mjumbe wa kikao hicho
Kamanda Kidavashari
alisema Baraza hilo
baada ya kujadiliana kwa muda mrefu
walibuliana kwamba kwakuwa jambo hilo
la imani za ushirikina linagusa
watu wengi kwenye kitongoji hicho Wazee hao walimuagiza mwenyekiti kuitisha mkutano wa wananchi wote ili
kuweza kuwabaini wahusika
Ndipo
hapo juzi kilifanyika kikao hicho cha wananchi wote na
kwenye kikao hicho walikuwa
wamemualika na mwenyekiti wa Kitongoji cha jirani cha Mpalamawe A Lucas
Mbutulo
Kidavashari alisema mara
baada ya kikao hicho kuanza
Mwenyekiti wa Kitongoji cha Mpalamawe
A LucasMbutilo alidakia na kumtaja
wananchi mmoja aliyekuwepo hapo
Lutha Wilisoni kuwa ndio mchawi
ambae amekuwa akisababisha vifo vya watu kwenye kitongoji hicho
Mwenyekiti
wa Kitongoji cha
Mpalamawe B Hilali
Rashid alimkaza Mwenyekiti wa Kitongoji cha Mpalamawe A
kutaja majina ya watu hadhalani
kuwa ni wachawi kwani anaweza
kusababisha hari ya uvunjwaji wa amani
Kamanda Kidavashari
alisema kitendo hicho cha kumkataza
Mwenyekiti wa Kitongoji cha
Mpalamawe A asiendelee kutaja majina ya
watu anao wadhania kuwa ni wachawi
kitendo hicho kiliwakasirisha wananchi hao na kuanza kumshambulia Mwenyekiti wao wa Kitongoji cha Mpalamawe B kwa kutumia silaha za jadi
Askari
Mgambo zaidi ya 20 wa Kijiji
cha Ikola walifika kwenye eneo hilo la mkutano na kumwokoa
Mwenyekiti huyo na
kumkimbiza hadi kwenye Kituo cha Polisi cha Ikola
kwa lengo la kumuhufadhi kwenye usalama
zaidi
Alisema kundi kubwa la watu ambao walikuwa
kwenye mkutano huo liliamua kwenda na walifika kwenye kituo cha Polisi cha Ikola
kwa lengo la kutaka kuvamia na
kuchoma moto kituo hicho cha polisi ili waweze kumpata Mwenyekiti huyo na kisha wamuuwe
Zoezi hilo hata
hivyo halikuweza kufanikiwa kwani
lilizimwa na Askari Polisi wa kituo hicho
kwa kushirikiana na Askari wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania Delti ya
Ikola
Alisema katika
tukio hilo Lutha
Wilison i ambae alitajwa kuwa ni mchawi
alijeruhiwa kwa kupigwa na
rungu na fimbo kichwani
na alikimbizwa katika Kituo
cha afya cha Ikola ambako
amelazwa na anaendelea kupatiwa matibabu huku hari yake
ikiwa ni mbaya
Kamanda
Kidavashari alisema watuhumiwa sita ambao wanashiliwa na jeshi la polisi
wanatarajiwa kufikishwa Mahakamani wakati wowote mara baada ya uchunguzi kukamilika
0 comments:
Post a Comment