Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Na Walter
Mguluchuma
Katavi
Kutokana na
Rushwa kuonekana kuwa
ni kikwazo katika
maboresho ya sekta ya Elimu
na sekta nyingine
hapa Nchini kwa ujumla
Serikali imekuwa akifanya
jitihada za kuhakikisha hali ya
Rushwa inakabiliwa hapa
Nchini Tanzania
Hayo yalisema
hapo jana na Afisa
kutoka ofisi ya takukuru
Mkoa wa Katavi
John Punju wakati
akiwa mada Rushwa
katika sekta ya
Elimu na athari
kwenye mkutano wa waalimu wa
shule zote za Msingi za
Manispaa ya Mpanda uliofanyika
katika shule ya Sekondari ya
Mtakatifu Maria mjini hapa
Alisema Serikali
imekuwa ikifanya jitihada kubwa
za kuhakikisha hari ya Rushwa
inakabiliwa na kutokomezwa
hapa nchini
Ambapo sheria
mwaka 1971 Sheria ya
kuzuia Rushwa NA 16 ilitungwa ikifuatiwa na
kikosi cha kuzuia Rushwa kilianzishwa mwaka 1975 kutokana na utumishi
wa umma kupanuka na watumishi
kwenda kinyume na
maadili ya kazi kwa kutumia
nafasi zao kama kitega
uchumi kutokana na hari ngumu ya uchumi
inayoikabili Taifa katika kipindi
hicho
John alieleza
kuwa mbali na
kutunga sheria hiyo
na kuundwa kwa kikosi
cha kuzuia Rushwa Serikali inaendelea
kufanya jitihada mbalimbali ikiwa
ni pamoja na kutunga sera
na sheria
Alifafanua kuwa ilikupambana na Rushwa serikali
ilianzishwa mwaka 1996 tume ya
Jaji Warioba ambayo imeonekana kuwa na mwanga wa mapambano dhidi ya Rushwa kwa kipindi hiki kutokana
na taarifa hiyo ya tume
baadhi ya viongozi wa ngazi za
juu Serikalini waliondolewa kwenye nafasi zao
na pia taasisi ya mapambano dhidi ya
rushwa imeimalishwa
Alisema athari
za rushwa ziko nyingi
sana ambapo alizitaja
baadhi ya athari hizo kuwa ni
Rushwa inachangia watu kuongozwa
na watu wasio na sifa na pia inapunguza uwajibikaji
katika kazi
Afisa huyo wa TAKUKURU alitaja athari nyingine kuwa ni Rushwa inachangia kushuka kwa Elimu na pia
inasababishia watu vifo na kuipotezea
Serikali pesa nyingi
Nae Afisa
Elimu wa Manispaa ya Mpanda Vicent
Kayombo alisema kuwa waalimu ni
wadau wakubwa katika mapambano
dhidi ya Rushwa hapa
nchini
Alisema kitendo
cha mtu kukataa kutowa taarifa kwa TAKUKURU
anapohitajika kufanya hivyo ni
kosa la jinai
Hivyo Kayombo
aliwataka waalimu wa Manispaa hiyo kutowa ushirikiano kwa TAKUKURU pindi wanapo kuwa
wanahitaji taarifa
Alisema
pia elimu hiyo iliyotolewa kwa
waalimu na Afisa wa TAKUKURU itasaidia sana kwenye jamii
kwani mwalimu mmoja anao
uwezo wa kuelimisha watu zaidi ya
elfu moja madhara ya Rushwa
0 comments:
Post a Comment