Home » » HOT NUUUUUUUUUZ: MWALIMU MSTAAFU(65) JELA KIFUNGO CHA MAISHA KWA KOSA LA KUMBAKA MJUKUU WAKE(5) SOMA HAPA MKASA MZIMA

HOT NUUUUUUUUUZ: MWALIMU MSTAAFU(65) JELA KIFUNGO CHA MAISHA KWA KOSA LA KUMBAKA MJUKUU WAKE(5) SOMA HAPA MKASA MZIMA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Na  Walter  Mguluchuma
Katavi
Mahakama ya Wilaya ya Mpanda  Mkoa wa Katavi  imemuhukumu  mwalimu mstaafu wa Shule ya Msingi Mpanda Ndogo Wilayaya ya Mpanda  Rashid  Mbogo  kifungo cha maisha jela baada ya kupatikana  na hatia ya kumbaka mjukuu  wake (5) na kumuharibu vibaya sehemu zake za siri
Hukumu  hiyo ilisomwa hapo leo   na Hakimu Mkazi  mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Mpanda  Chiganga Ntengwa  baada ya mahakama kuridhika na ushahidi  uliotolewa mahakamani hapo na pande zote mbili za mashitaka  na  utetezi
 Awali katika kesi hiyo mwendesha mashitaka  Godfrey  Rwezabila  alidai mahakamani kuwa mshitakiwa  Rashid  Mbogo  alitenda kosa hilo oktoba 19 mwaka  jana majira ya saa mbili  na nusu usiku nyumbani kwake huko  katika Kijiji  cha majalila Wilayani  hapa
Siku hiyo ya tukio mshitakiwa  alidaiwa  kumbaka mjuu kuu wake huyo  wakati akiwa amelala  chumbani kwenye godoro  wakati akiwa amelala  na mtoto wake na Rashid Mbogo aitwaye  Faraji  Mbogo(9) ambae alishuhudia   wakati baba yake akimbaka mtoto huyo
 Ilielezwa mahakamani na mwendesha mashitaka kuwa  siku  hiyo  mke wa mshitakiwa  alimuuga  mume wake kuwa anakwenda kwenye zizi la  mbuzi lililokuwa jirani na nyumbani kwao kufungia mbuzi  ndipo alipotumia nafasi hiyo ya kuingia chumbani  na  kumkuta mjuu kuu wake akiwa amelala na mtoto wake na kisha alimshika na kuanza kumbaka  huku mtoto wake wa kuzaa mwenyewe akiwa anashudia tendo hilo
 Alieleza  mshitakiwa aliweza kukamatwa siku hiyo hiyo na majirani zake  ambao walimpeleka hadi kituo cha polisi cha Wilaya ya Mpanda  huku mjukuu wake  nae alikimbizwa kwenye hospitali ya Wilaya ya Mpanda kwa ajiri ya kupatiwa matibabu  baada ya kuwa ameharibiwa vibaya kwenye sehemu zake za siri

Mshitakiwa katika utetezi wake  ambapo hakuna  na  shahidi  hata mmoja  huku upande wa mashitaka ukiwa na mashahidi sita akiwepo mtoto wake  mwenyewe  Faraji  Mbogo alikana kutenda kosa hilo kabisa kwalealicodai mahakamani hapo  kuwa umri wake ni mkubwa na kwa sasa ameishaishiwa nguvu za kiume hivyo asingetenda kosa hilo
Baada ya utetezi huu mahakama iliamuru mshitakiwa akapimwe hospitalini ili baini  kama kweli hana  nguvu za kiume ambapo majibu ya daktari yalionyesha kuwa Rashid  Mbogo  bado  anazo mbegu za kiume zinazomfanya atende tendo la  ndoa
Hakimu  Chiganga  baada ya  kurudhika na ushahidi uliotolewa  aliiambia  mahakama kuwa mshitakiwa amepatikana na  kosa la kifungu cha  sheria  namba 130 na 131 cha   marekebisho ya sheria ya mwaka 2009
Akisoma hukumu hiyo alisema kutokana na kuapatikana na kosa hilo bila  mashaka yoyote mahakama  imemuhukumu  Rashid  Mbogo kutumikia kifungo cha maisha jela kuanzia jana

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa