Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Na Walter Mguluchuma
Katavi
Waziri Mkuu Mizengo Pinda amewataka wananchi kujitokeza
kujiandikisha katika daftari la kudumu la wapiga kura ili waweze kupata nafasi
ya kushiriki katika uchaguzi mkuu ujao itakapofika hapo oktoba 25 mwaka huu.
Waziri Mkuu Pinda ameyasema hayo juzi mara baada ya kujiandikisha kwenye kituo cha
kupigia kura ofisi ya Mtendaji wa Kata
ya Kibaoni ililiyoko Wilaya ya Mlele Mkoani Katavi.
Amsema iwapo watajiandikisha watapata haki ya kuweza
kushiriki katika uchaguzi Mkuu wa Rais, wabunge na Madiwani unaotarajia
kufanyika nchini kote.
“Ninawasihi
Watanzania wote tusiache kutumia fursa hii ,kila mtu ahakikishe kuwa
anajiandikisha, Ni fursa pekee itakayohakikisha kila mwananchi anashiriki
uchaguzi wa kumpata Rais, Mbunge na Diwani,” alisema Waziri Mkuu Pinda.
Waziri
Mkuu alisema amefarijika kwa kazi aliyoiona ikifanyika kwani hadi sasa
Halmashauri za Nsimbo na Mlele zimefanikiwa kuandikisha watu kwa zaidi ya
asilimia 100.
Naye
Mkurugenzi wa Tume ya Uchaguzi Taifa Julius Mallaba ameeleza kuwa hakuna mtu
atakayeshindwa kuandikishwa katika zoezi linaoendelea kila aliyepo kwenye kituo
lazima ataandikishwa.
Awali akiwasilisha taarifa ya uandikishaji
katika Halmashauri ya Mlele, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Godwin Benne alisema walilenga kuandikisha
watu 19,482 lakini hadi kufikia jana walifanikiwa kuandikisha watu 20,292 sawa
na asilimia 105. Uandikishaji katika wilaya ya Mlele ulianza tarehe 18 Mei,
mwaka huu.
“Mlele tuna vituo 84 katika tarafa tatu za
Inyonga, Mpimbwe na Mamba. Inyonga tuna vituo 28, Mpimbwe viko 23 na Mamba viko
33.
Akifafanua zaidi, Bw. Benne alisema katika
kata ya Kibaoni ambayo ina vituo sita, juzi peke yake walifanikiwa kuandikisha
watu 1,007 kikiwemo kituo cha Kibaoni ambacho Waziri Mkuu Pinda alijiandikisha.
Alivitaja vituo vingine kuwa ni Milumba,
Sungusungu, Ilalangulu, Manga na Shule ya Msingi Kakuni ambako Mama Tunu Pinda
alijiandikisha jana hiyo hiyo.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya
Wilaya ya Nsimbo, uandikidhaji katika
Halmashauri ya Nsimbo uandikishaji ulianza Mei 18, 2015 kwenye kata 12 na
kwamba hadi kufikia jana, kata nne zilikwishaandikisha watu 12,001 sawa na
asilimia 108.9 licha ya kuwa matarajio yao yalikuwa ni kuandikisha watu 11,014.
Alizitaja kata hizo kuwa ni Nsimbo, Kapalala, Magamba na Uruwira.
Kwa upande wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda
hadi kufikia mwishoni mwa wiki walikuwa wameandishwa jumla ya wapiga kura
14,972 sawa na asilimia 94.6 na lengo waliweka lengo la kuandikisha wapiga kura
15,824 katika tarafa moja ya Karema walikoanzia kwenye kata za Ikola,Karema na
Kapalamsenga kisha watanza kuandikisha maeneo mengine yaliyobakia ya Tarafa ya
Kabungu ,Mwese.
Zoezi la uandikishaji
kuboresha daftari la kudumu la
wapiga kura linaendelea Mkoani Katavi na maeneo mengine nchi,ambapo wananchi
Mkoani Katavi wamehamasika kujitokeza kwa wingi kwenye zoezi hilo hali
inaopelekea wananchi wengine kukesha kwenye vituo vya uandikishaji ili waweze
kupata nafasi ya kuwahi kuandikishwa.
mwisho
0 comments:
Post a Comment