Home » » MZEE WA WA BARAZA AFIKISHWAMAHAKAMANI KWA KOSA LA KUOMBA RUSHWA

MZEE WA WA BARAZA AFIKISHWAMAHAKAMANI KWA KOSA LA KUOMBA RUSHWA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Na  Walter  Mguluchuma
Katavi 
Taasisi  ya  kuzuia  na kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Katavi  imemfikisha  katika  mahakama ya Wilaya ya Mpanda na kumfungulia mashitaka mzee wa  baraza wa Mahakama ya mwanzo  ya Mpanda Anna  Mlugala kwa  tuhuma za  kosa la  kuomba na kupokea  rushwa ya shilingi laki moja kinyume na kifungu cha sheria  ya kuzuia  na kupambana na Rushwa Na11 ya mwaka 2007
Mkuu wa  TAKUKURU wa Mkoa wa Katavi john Minyenya  aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa  mhumiwa  alikamatwa hapo mei  21 mwaka huu katika eneo la Mtaa wa Makanyagio Mjini hapa kufutia mtego ulikuwa umaandaliwa na TAKUKURU
Alieleza  mshitakiwa  kwa kutumia nafasi yake ya uzee wa baraza   wa Mahakama ya mwanzo  anadaiwa  kutenda kosa  la kumshawishi na kumwomba  rushwa  ya shilingi laki moja  kutoka kwa msiri  mmoja  ili  aweze  kutowa  upendeleo  wa kumsaidia  katika kesi  yake  Na 21\2015
 Alieleza  baada ya TAKUKURU  kupata taarifa hizo  ilianza kufanya uchunguzi  wa awali na ndipo  waliweza kubaini  tuhuma hizo  ni za kweli
Minyenya  alisema  uchunguzi   huo uliofanywa  uliweza  kuthibitisha  kuwepo kwa kesi  hiyo  na kwamba  mshitakiwa  Anna Mlugala  alikuwa na  na mawasiliano  na msiri
Ndipo terehe 21  mei    TAKUKURU  waliandaa mtego wa Rushwa  dhidi ya  mshitakiwa  na waliweza kumkamata  huko katika Mtaa wa Makanyagio mjini hapa
 Alieleza  baada ya  mtuhumiwa kufikishwa  mahakamani  alisomewa  mashitaka yanayo  na alikana  mashitaka dhidi yake  ambapo dhamana ilikuwa wazi  na mshitakiwa aliweza  kutimiza  masharti ya  dhamana  na  yuko nje  hadi hapo  kesi yake  itakapo tajwa tena june  6 mwaka huu
TAKUKURU Mkoa wa Katavi  inatowa  wito kwa wananchi  kuzingatia  maadili  na kutojihusisha na vitendo  vya Rushwa  wakati wa kutekeleza majukumu yao  ya kila siku  na wakati wanapo   dai haki zao  kwani  Rushwa  ni adui  haki  hivyo haikubaliki

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa