Na
Walter Mguluchuma
Katavi
Watu
watatu Charles Manyanye (55) Jacob Charles (28)
na Mussa Mwigize (30) wakazi wa Kitongoji cha
Kamigusu Wilaya ya Mpanda wamekamatwa kwa tuhuma za
kukutwa wakiwa na silaha mbili Bunduki aina ya Gobole
wanazimiliki kinyume cha sheria
Watuhumiwa
hao wote watatu walikamatwa machi 28 mwaka huu majira ya
saa kumi na moja jioni huko katika Kitongoji
cha Kamigusu Wilaya ya Mpanda
Kamanda wa
Polisi wa Mkoa wa Katavi Dhahiri Kidavashari alisema
watuhumiwa hao walikamatwa kufuatia msako unaofanywa na jeshi la polisi
Mkoa wa Katavi dhidi ya watu wanao miliki silaha kinyume
cha sheria
Alisema
kabla ya Polisi kuwakamata watuhumiwa hao jeshi hilo lilikuwa
limepata taarifa kutoka kwa Raia wema kuwa kuna watu watatu
wanamiliki silaha isivyo halali kwenye Kitongoji cha Kamigusu
Kidavashari
alisema mbele ya waandishi wa habari ndipo hatua za haraka
zilichukuliwa kwa polisi kufika Kijijini hapo
kwenye nyumba za watuhumiwa hao watatu
Alisema
baada ya kufika polisi walipofanya upekuzi kwenye
nyumba walizokuwa wakiishi watuhumiwa na waliweza
kuwakuta watuhumiwa wakiwa na silaha mbili
bunduki aina ya Gobole moja ikiwa imefishwa juu ya dari
na nyingine kwenye uvungu wa kitanda
Kamanda
Kidavashari alieleza watu wote watatu bado wanaendelea
kushikiliwa na polisi kwa mahojiano zaidi na wanatarajiwa
kufikishwa mahakamani mara baada ya uchunguzi utakapokuwa umekamilika
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
0 comments:
Post a Comment