Na Walter
Mguluchuma
Katavi
Mkuu wa Mkoa wa
Katavi Dr Ibrahimu Msengi amezindua mradi
wa huduma ya uzazi wa Mpango inayotolewa bure na Marie Stopes
Tanzania (MST) kwa Wananchi wa
Mkoa wa Katavi
Uzinduzi huo
uliohudhuliwa na maelfu ya wakazi wa Mkoa wa Katavi ulifanyika jana katika
uwanja wa shule ya Msingi
Kashaulili mjini Mpanda ambapo
kaimu Mkuu wa Mkoa ambae ni mkuu wa Wilaya ya Mpanda Paza
Mwamlima alizindua huduma ya mpango huo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Katavi Dr Ibrahimu Msengi
Dr Msengi
katika hotuba yake alisema kuwa
uzazi wa mpango ni hiari ambao mtu
au wanandoa wanaamua idadi
ya watoto watakao zaa kwa
mpangilio uliokubalika kwa ajiri ya afya zao
Alisema huduma hiyo ya mpango wa uzazi iliyozinduliwa
katika Mkoa wa Katavi mpango huo utasaidia
kupunguza vifo vya akina
Mama na watoto katika Mkoa wa Katavi na watoto
chini ya umri wa miaka
mitano ikiwa ni katika kutimiza
malengo ya milenia namba nne
na namba tano
Alifafanua zaidi
ya wanawake elfu nane hufa hapa
nchini kila mwaka kutokana na uzazi na kinachoshangaza wanawake
walioolewa ndio wengi wao
wamekuwa wanashindwa kupata huduma ya uzazi wa mpango
Alisema wananchi wa
Mkoa wa Katavi watumie fursa
hiyo kuwahamsisha watu watumie
njia za uzazi wa mpango
kwani ni salama
Dr Msengi aliwataka wananchi
wawatumie wataalamu ili
waweze kuwapatia ushauri na kuwaelimisha
umuhimu wa uzazi wa mpango na
kuwapuuza watu ambao
wanatafsiri vibaya huduma ya
mpango wa uzazi na wanaopinga
uzazi wa mpango
Aliisema
kumekuwepo na imani potofu
na taarifa zisizo sahihi kuhusu
uzazi wa mpango ambazo
zimesababisha kina mama wengi
kuwa waoga wa kutumia njia
hizo na kishia kushika mimba
zisizotarajiwa
Kwa wanaume njia ya
za uzazi wa mpango ni
chache kwa hiyo fursa
ya kushiriki ni ndogo ukilinganisha na wanawake hata hivyo
kuna baadhi ya wanaume
huwazuia wake zao kutumia uzazi wa mpango kufanya hivyo ni
kutomtendea haki mwanamke
Alisema wanaume wamekuwa wakidhani kuwa jukumu
la kunga kizazi na mpango wa
uzazi ni kwa ajiri ya mwanamke
tuu wakati jukumu hilo ni la mwanaume na mwanamke hivyo huduma hiyo waakikishe inawafikia wananchi
wote wa Mkoa wa Katavi hata yale maeneo ambayo yamekuwa yakifikika kwa shida
kama vile Ilunde Bugwe, Mnyagala ambako unakuta mtu mmoja anakuwa na watoto 40
wa kuzaa mwenyewe na wake zaidi ya watatu
Nae Mkurugenzi wa Rasilimali watu wa Marie
Stopes Tanzania Eliy
Reweta alisema pamoja na kuendeleza
kazi zilizokuwa huko nyuma timu
za utoaji huduma zimeongezwa
katika mikoa ya Singida ,
Kilimanjaro ,Manyara na Katavi
lengo ni kumfanya kila mtu achague
njia ya uzazi ya mpango anayohitaji
Alisema
huduma zinazo tolewa kupitia
shirika la Marie Stopes Tanzania zinachangia asilimia ishirini na tano yahuduma
zote za mpango wa uzazi
ukiondoa kondomu
Alifafanua kuwa huduma ya uzazi wa mpango hutolewa na timu ya
wataalamu wa uzazi wa mpango waliopitia
mafunzo maalumu na kila timu inagari linalozunguka
na kutowa huduma hizo katika Zahanati na
vituo vya afya vilivyoko
katika maeneo ya vijijini kwa siku 21
kila mwezi
Nandio maana kwa
kutambua umuhimi huo Marie Stopes imekabidhi gari jipya wakati wa uzinduzi huo
kwa ajiri ya Mkoa wa Katavi litakalo saidia kutowa huduma na kuwafikia kila mtu mahari pale alipo alisema Elly
Mwenyekiti wa
Halmashauri ya Mji wa Mpanda Enock Gwambasa alieleza kuwa mpango huo utasaidia kuwafanya watu waweze
kuwa na utatatibu mzuri wa kuzaa
watoto kwa mpangilio kuliko iliyo sasa
Alisema Mkoa wa Katavi ni miongoni mwa mikoa
miwili inayoongoza kwa kuwa na ongezeko kubwa la watu ikiwa inaufuatia Mkoa wa Dares salaam
Kwa upande wake mrembo wa
mashindano ya Miss Marie
Stopes Tanzania Doreen
Benne alisema kuwa uzazi wa mpango unamkinga mtu
kupata mimba zisizotarajiwa na kumwepusha
na kuingia kwenye mtego wa kutoa mimba
kusiko salama
Pia wanawake wengi kwa sasa kupitia mpango huo wa uzazi wanafanikiwa kumaliza masomo yao na
kutengeneza maisha kabla ya kuanza
mpango wa kutengeneza familia
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
0 comments:
Post a Comment