Home » » HATARI KISA WIVU WA MAPENZI: MWANAMKE (25) AJINYONGA KWA KITENGE HADI KUFA .

HATARI KISA WIVU WA MAPENZI: MWANAMKE (25) AJINYONGA KWA KITENGE HADI KUFA .

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Na   Walter  Mguluchuma
Katavi yetu blog
Mwanamke mmoja Mkazi wa Kitongoji cha Mtisi Kata ya Sitalike Wilaya  ya  Mlele Mkoa wa Katavi amejinyonga  hadi kufa kwa kutumia  kitenge chake kutokana na wivu wa kimapenzi.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi Dhahiri  Kidavashari aliwaambia  waandishi wa   habari kuwa mwanamke huyo aliyejinyonga    hadi kufa alifahamika kwa jina la Milembe  Charles (25)  Mkazi wa Kitongoji  cha Mtisi.

 Alisema tukio la mwanamke  huyo kujinyonga  lilitokea  hapo  jana  majira ya saa kumi na mbili   jioni  katika shamba la wazazi wake lililopo kijini hapo.

 Alifafanua kuwa  kabla ya tukio hilo marehemu alikuwa akiishi nyumbani kwa wazazi wake  baada ya kuwa wametengana  na mume wake  ambae walikuwa  na ugomvi nae kufuatia  mume wa marehemu kuwa na mke mwingine kwenye Kijiji cha Kasekese  kitendo ambacho marehemu hakuwa ameridhishwa nacho.

 Siku hiyo ya tukio marehemu  alikuwa  alikuwa  nyumbani kwa wazazi wake ndipo ilipofikia mida hiyo ya tukio aliondoka nyumbani kwa wazazi wake pasipo kuwa amewaagakuwa anakwenda wapi.

 Alisema wazazi wa marehemu  baada ya kuona muda umekuwa mrefu  tokea marehemu alipoondoka nyumbani walipata mashaka  na ndipo walipoamua kwenda nyumbani kwa mume wake kumtafuta hata hivyo mume wa marehemu aliwajibu kuwa siku hiyo alikuwa haja fika nyumbani kwake. 
 
Jitihada za kumtafuta  ndipo zilianza na ndipo waliweza kumkuta marehemu akiwa amejinyonga hadi kufa  juu ya mti  wa mwembe  kwa kutumia kitenge chake  katika  kichaka  kilichopo jirani na nyumba  ya wazazi wake.

Kidavashari    alisema  uchunguzi wa tukio hilo umebaini   kuwa  chanzo cha  tukio hilo ni   wivu wa mapenzi  kutokana na mume wa marehemu kuwa na  mahusiano ya kimapenzi na mwanamke mwingine   na mwili wa marehemu  umeishafanyiwa  uchunguzi wa kidaktari na  wamekabidhi  ndugu  wa marehemu kwa ajili ya mazishi.


0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa