Na Walter
Mguluchuma
Katavi
Wananchi wa Kijiji cha Ibindi Kata ya Machimboni Wilaya ya Mlele
Mkoa wa Katavi wamevamia kambi ya Kanpuni ya uchimbaji wa madini ya Sambulu Mining na kuchoma moto
gari la Kampuni hiyo na vitu mbalimbali baada ya watumishi wa Kampuni hiyo kumkamata
mwanajijiji mwenzao na na kisha kumkata na panga kwa kumtuhumu kuiba mawe yanayosadikiwa kuwa na madini ya
Dhahabu yenye kilo mbili ya thamani ya milioni 90
Kwa mijibu wa
Diwani wa Kata hiyo Raphael Kalinga tukio hilo lilitokea hapo juzi
majira ya saa kumi na nusu usiku Kijijini hapo
Siku hiyo ya tukio watumishi wa Kampuni hiyo
wakiwa na msimamizi wa Kampuni hiyo
aitwaye Seif Hamad walifika
kwenye Kijiji hicho huku wakiwa wameshika mapanga na kuwafunguza baadhi ya
wanakijiji ambao walikuwa wakiwatuhumu
kuwa wamewaibia mawe ambayo wanadai yalikuwa yana madini ya dhahabu kilo
mbili
Katika msako huo walioufanya watumishi
hao waliwajeruhi wananchi saba kwa kuwakata kata na mapanga
katika sehemu zao za mwili
Baada ya kuwa wamewajeruhi watumishi hao walimchukua wanakijiji mmoja aitwaye Rongino Petro
na kwenda nae kwenye kambi ya Kampuni hiyo iliyoko nje kidogo ya
kijiji hicho
Alisema
wananchi walivyoona mwenzao
amechukuliwa waliamua kwenda
kwenye kambi ya kampuni hiyo huku wakiwa wameongozwa na Mwenyekiti wa Kijiji Cristopher Modesti na Mtendaji wake wa Kijiji
Sulvia Kampama kwa lengo la kumkomboa mwenzao
Hata hivyo baada ya kuwa wamefika kwenye kambi
hiyo viongozo hao wa Kijiji pamoja na wananchi hao waliambiwa ni marufuku
kusogea kwenye eneo hilo na waondoke mara moja
Diwani Kalinga alieleza baada ya muda mfupi
baadaye polisi watatu walifika Kijijini hapo
huku wakiwa na gari lao na
kuwakamata wananchi saba ambao waliokuwa wamejeruhiwa na watumishi hao
kitendo hicho kiliwaudhi wananchi wa Kijiji hicho kwa kile walichodai kuwa
wananchi hao hawakuhusikaa na wizi huo
Alisema wanakijiji hao walianza kuwashambulia polisi kwa
mawe wakitaka wananchi wenzao
waachiliwe na polisi walipoona wamezidiwa waliamua kuondoka kwenye eneo hilo huku
wakiwa wamewabeba kwenye
gari lao wana kijiji hao saba ambao waliwapeleka kwenye kituo cha Polisi
cha Mpanda Mjini
Kundi kubwa la wanajikiji baada ya kuona wenzao wembebwa na Polisi walielekea kwenye Kambi ya Kampuni hiyo huku wakiwa wameshika mikononi silaha za
jadi hari ambayo iliwafanya watumishi wa kampuni ya Sambulu watimue mbio
na kuicha kambi ikiwa haina mtu hata mmoja
Alisema
wanakijiji hao mbao welikuwa na hasira waliamua kuchoma gari aina ya Toyota yenye namba za usajiri T531 AGT na kuiteketeza kabisa kwa moto kila
waliharibu vitu mbalimbali vya Kampuni hiyo
na kisha walikwenda kuvitupa na kisha
walitamka kuwa mwekezaji huyo
asionekane tena kwenye Kijiji hicho
Alieleza kuwa
katika tukio hilo watu saba wanashikiliwa na polisi kuhusiana na tukio hilo ambao ni
Rongino Petro,Sokoni Mteta, Taji Sanane ,Kulwa Jamres,Gabrieshi Shaulitanga ,Malilo Pelesiano
na mtu mmoja aliyefahamika kwa
jina la Mussa
Kwa upande wake
Mwenyekiti wa Kijiji hicho
Cristophar Modesti alisema kuwa wananchi wa Kijiji hicho mara
baada ya kutokea kwa tukio hilo wamekimbia familia zao kwa kuhofia kukamatwa na polisi
Nae Katibu
wa Mbunge wa Jimbo hilo la Katavi
Charles Kanyanda linaloongozwa na Waziri
Mkuu Mizengo Pinda alilazimika jana kwenda kijijini hapo na kufanya mkutano na
wananchi ambapo aliwaeleza kuwa
kungekuwa na mahusiano mazuri baina ya
wanakijiji na mwekezaji hayo yasingetokea
Pia aliwaomba wananchi wa Kijiji hicho
wapunguze hasira kwa mwekezaji huyo na
aruhusiwe aendelee kufika
kijijini hapo wakati uchunguzi wa tukio hilo ukiwa bado unaendelea
Mkuu wa Wilaya ya
Mlele Kanali Ngemela Lumbinga amekili kupokea taarifa za tukio hilo la wananchi
kuvamia kambi hiyo na kuchomwa kwa gari la kampuni hiyo
Alisema
anatarajia kufika kwenye eneo hilo huku
akiwa na Afisa wa madini ilikuweza kuongea na wananchi wa kijiji hicho cha
Ibindi
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
0 comments:
Post a Comment