Home » » MADIWANI NSIMBO MAKAMPUNI YA MADINI YAWEYANALIPOTI KWENYE VIJIJI KABLA YA KUANZA KUCHIMBAMADINI

MADIWANI NSIMBO MAKAMPUNI YA MADINI YAWEYANALIPOTI KWENYE VIJIJI KABLA YA KUANZA KUCHIMBAMADINI


Na Walter  Mguluchuma
Katavi
 Baraza la Madiwani wa Halimashauri  ya Nsimbo  Mkoani Katavi  limeyataka  makampuni  ya uchimbaji wa madini  yanayokuja kufanya  utafiti na kuchimba madini   kwenye  maeneo ya Halimashauri  hiyo yawe yanakwenda    kuripoti  kwenye uongozi wa  Serikali ya kijiji  husika kabla hawajaanza kufanyashughuli
Baraza la Madiwani  lilitowa  kauli hiyo hapo juzi kwenye kikao cha baraza la madiwani  wa Halimashauri hiyo kilichofanyika  kwenye ukumbi wa  Halimashauri ya Nsimbo
Diwani wa  Kata  wa Kata ya Magamba Philipo  Kalyalya  alikuwa  ndio  mchangiaji wa kwanza  kutowa malalamiko kwenye Baraza hilo  kuhusiana na makampuni ya uchimbaji wa madini
Alisema  imekuwa ni tabia ya makampuni yanayofanya utafiti na uchimbaji wa madini kwenye  Halimashauri hiyo  kufanya shughuli hizo bila  kulipoti kwenye uongozi wa Serikali  za vijiji husika na matokeo yake kumekuwa na migogoro ya mara kwa mara  baina ya makampuni na  wanchi
 Alifafanua  hata Halishauri yake ya Nsimbo  haifahamu  idadi ya makampuni yanayofanya shughuli   kwa kuwa  makampuni hayo yanakuja na kuanza shughuli  hata  huwa hayatowi taarifa kwenye Halimashauri
Diwani wa Kata ya Machimboni Raphael Kalinga alieleza kuwa  katika eneo la Mkoa wa Katavi  Halimashauri ya Nsimbo  ndio kunako patikana madini kuliko maeneo mengine ya Halimashauri za Mkoa wa Katavi lakini wameshindwa kunufaika na makampuni ya uchimbaji wa madini
 Alisema yapo makampuni yamekuwa yakipewa leseni za utafiti wa kuchimba  madini    lakini badala ya kufanya shughuli za utafiti  wamekuwa  wakifanya  shughuli  za  chimba madini   badala ya utafiti

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa