Home » » HATARI WATU WANNE WANASHIKIRIWA NA POLISI KWA TUHUMA ZA KUCHINJA MTU

HATARI WATU WANNE WANASHIKIRIWA NA POLISI KWA TUHUMA ZA KUCHINJA MTU



Na Walter Mguluchuma Mpanda Katavi yetu blog
POLISI mkoani Katavi  inawashikilia  watu wanne wakituhumiwa kumua kikatili mkazi wa kijiji cha Kaseganyama, Kata ya Sibwesa  wilayani Mpanda, Salu Kadigosa (65) kwa kumchinja kwa imani za kishirikina .


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Katavi ,  Dhahiri Kidavashari  akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake  amethibitisha kutokea kwa tukio hilo ambapo  amewataja  watihumiwa  hao kuwa ni pamoja na Masanja Kisatya (32) , Silya Masunga (30) wote wakazi wa kijiji cha Kaseganyama.

Wengine  kwa mujibu w Kamandawa polisi wa Mkoa wa Katavi   ni pamoja na Kibya Malongo (27)  na Lutelema Mwanza (33) wote wakiwa  wakazi wa kijij cha Sibwesa  wilayani humo .


Anasimulia mkasa huo uliotokea Agosti 18, mwaka huu, saa mbili usiku kijijini Kaseganyama, KamandaKidavashari  alida kuwa uchunguzi wa awali umebainisha kuwa marehemu alikuwa akilalamikiwa na na ndugu zake  kwamba ni mchawi.

Kwa mujibu  wa Kidavashari , mwaka 1993 mtoto wa marehemu  aitwae Masanja Kisatya (32) alifiwa na watoto  wawili , Rebeka Msanja na Sayi Masanja pia kaka yake mkubwa  alifiwa na watoto  watatu , ndipo wanafamilia waliketi  na kuamua kwenda kwa mganga  wa kienyeji .

“Ndipo mganga  huyo wa kienyeji alipomtaja marehemu   kuhusika na vifo vya watoto hao kwa imani za kishirikina” anadai Malengo
.
Inadaiwa kuwa Agosti 16, mwaka  huu saa  kumi na mbili jioni  mtu  aliyetambulika kwa jina moja la Lugalila , mkazi wa  kiji cha  Sibwesa akiwa na mwenzake wawili ambao  hawakufahamika majina yao waliwasili nyumbani kwa Masanja Kisatya .

Kwa mujibu  waKidavashari muda mfupi  baadae wageni hao  waliondoka wakiongozana namwenyeji wao Masanja  akiwasindikiza kwenda kuwaonesha nyumbani kwa Salu Kadigosa  kisha Masanja akarejea kwake .

“Muda mfupi  baadae  mauaji hayo ya kutisha  yalitokea  na Masanja  lipewa taarifa lakini hakuchukua hatua yeyote hali iliyoashiria kuwa yeye ndiye aliyehusika kwenye mauaji hayo’ anadai Malengo . 

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa