Home »
» AUWA KWA KUPIGWA NA KITU KIZITO KICHWANI WAKATI AKIELEKEA KUNUNUA MAGUNIA YA MPUNGA
AUWA KWA KUPIGWA NA KITU KIZITO KICHWANI WAKATI AKIELEKEA KUNUNUA MAGUNIA YA MPUNGA
Na Walter Mguluchuma
Mpanda Katavi
Mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Enock Lugonda (35) Mkazi wa Kijiji cha Mbugani Kata ya Kakese Wilaya Mkoa wa Katavi ameuwawa kwa kupingwa na kitu kizito kichwani na watu wasiofahamika wakati akiwa njiani anaelekea kununua gunia 40 za mpunga
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi Kamishina mwandamizi msaidizi Dhahiri Kidavashari tukio hilolimetokea hapo Agosti 17 majira ya saa saba mchana
Kidavashari alisema siku hiyo ya tukio marehemu aliondoka nyumbani kwake majira ya saa saba mchana akiwa na mtu mmoja asiyefahamika na kuelekea katika kitongoji cha Mwagoe kwa lengo la kwenda kununua mpunga gunia 40
Baada ya kuondoka marehemu hakurejea tena nyumbani hadi majira ya saa kumi jioni alipookotwa akiwa ameisha fariki Dunia katika eneo la barabara itokayo Kijiji cha Kakese kuelekea Kijiji cha jirani cha Mwamkulu
Alieleza baada ya marehemu kuokotwa akiwa amefariki Dunia wananchi walitowa taarifa kwa jeshi la polisi ambao walifika kwenye eneo hilo na kisha marehemu alifanyiwa uchunguzi wa kidakitari na kubaini kifo chake kilisababishwa na kupingwa na kitu kizito kichwani
Kamanda Kidavashari alisema jeshi la polisi linamshikilia Mussa Robart (29) Mkazi wa kijiji cha Mbugani Kata ya Kakese kwa tuhuma za mauwaji hayo
Alieleza kwani ndiye mtu ambae alikuwa na mahusiano ya kibiashara na marehemu na ndiye waliyewasiliana na marehemu kwa njia ya simu kuhusiana na biashara hiyo ya mpunga
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
0 comments:
Post a Comment