Home »
» Shirika la Walter Red latoa msaada wa pikipikim 24 za thamani ya zaidi ya tsh 52, kwa ajiliya kutolea huduma za Afya
Shirika la Walter Red latoa msaada wa pikipikim 24 za thamani ya zaidi ya tsh 52, kwa ajiliya kutolea huduma za Afya
Na Walte Mguluchuma
Mpanda Katavi
Shirika la Walter Red limetowa msaada wa Pikipiki 24 zenye thamani ya Tsh 52,800,000 kwa Halmashauri za Mkoa wa Katavi kwa ajiri ya kutolea huduma za afya ili kusaidia ufutiliaji wa wagonjwa watoro wanaotumia dawa za kufubaza makali ya Virusi vya VVU Mkoani Katavi
Pikipiki hizo zilikabidhiwa mwishoni mwa wiki iliyopita kwa Halmashauri zote nne za Mkoa wa Katavi katika hafla iliyofanyika katika viwanja vya ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Katavi ambapo mgeni Rasmi alikuwa ni Mkuu wa Mkoa wa Katavi Dr Rajabu Rutengwe
Katika Risala iliyosomwa na Mganga Mkuu wa Mkoa wa Katavi Dr Yahaya Hussein kabla ya makabidhiano hayo alisema vitendea kazi hivyo vitasaidia kufanyanyia kazi katika maeneo mawili kwa ajiri ya kutolea huduma za Afya
Alisema pikipiki hizo zitawasaidia ufuatiliji wa wateja wanao tumia dawa za kufubaza VVU ambao watakuwa na kupindi cha miezi mitatu mfululizo bila kufika kwenye vituo vyao walivyokuwa wakichukulia dawa
Alifafanua lengo ni kupunguza na hatimaye kutokomeza kabisa utoro wa watu wanao tumia dawa za kufubaza VVU utoro huo umekuwa ukiongezeka siku hadi siku katika Mkoahuu
Dr Yahaya Hussein alieleza wataweza kutowa huduma ya kuzuia maambukizi toka kwa mama kwenda kwa mtoto yaani wamelenga kuongeza maeneo ya kutolea huduma kwenye maeneo ambayo hayakuwa na kituo cha kutolea huduma hivyo wataoa huduma ya Mkoba
Pia zitasaidia kusafirisha sampuli za damu (DBS ) toka sehemu moja hadi nyingine na hatimaye zipelekwe maabara kubwa ya Mbeya ilikubaini maambukizi ya toka kwa mama kwenda kwa mtoto
Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Katavi Dr Rajabu Rutengwe alisema msaada huo uliotolewa na shirika la Walter Red Program HJFMRI ni ushahidi tosha kwamba shirika hilo linania njema ya kuisaidia Serikali hasa katika Wizara ya Afya na ustawi wa jamii
RC alisisitiza kwamba pikipiki hizo zitumike kwa ajiri ya shughuli za afya na hususani za Ukimwi na sivinginevyo na watumiaji watambue hivyo si kwa matumizi yao banafsi
Aliwaagiza Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi kuhakikisha wanawachukulia hatua za kinidhamu wale wote ambao watabainika kutumia pikipiki hizo kwa matumizi yasiyokusuhudiwa
Mkoa wa Katavi unazo jumla ya Halmashauri nne ambazo ni Mpanda Mjini Nsimbo , Halmashauri ya Wilaya ya Mlele na Halmashauri ya Nsimbo ambapo kila halmashauri imepatiwa Pikipiki sita
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
0 comments:
Post a Comment