Na Walter
Mguluchuma
Mpanda Katavi
Watu wanane
wanaosadikiwa kuwa majambazi wakiwa na siraha za jadi
mapanga na marungu wamevamia
kambi ya Kampuni ya
wachina wanaotengeneza Barabarakwa kiwango cha rami ya kutoka Mpanda hadi
Sitalike Wilayani Mlele Mkoa wa Katavi na kumjeruhi
mlinzi wa Kampuni hiyo
Kwa mujibu wa Kamanda
wa Jeshi la Polisi wa Mkoa
wa Katavi Kamishina
mwandamizi msaidizi Dhahiri Kidavashari alisema tukio
hilo lilitokea hapo
Aprili 22 mwaka huu majira ya saa
tano na
dakika thelathini na
tano usiku katika
kambi ya kampuni hiyo iliyoko katika
Eneo la kata ya Magamba Wilaya ya Mlele Mkoa wa Katavi
Alisema siku
hiyo ya tukio watu hao
wanane wanaosadikiwa kuwa
ni majambazi walifika
kwenye kambi hiyo
na kisha walimvamia
mlinzi wa kampuni hiyoj
Joseph Sarangi na
kumshambulia kwa kutumia silaha za
jadi mapanga na
marungu na kumjeruhi
kwenye paji la uso na kichwani kufanikiwa kuiba betrii
la gari aina ya
Nissan lenye Namba
120 na kisha kutokomea
kusikojulikana
Alieleza kuwa
jeshi la Polisi
lilipata taarifa ya tukio hilo
baada ya muda mfupi
baada ya kuwalimetokea
kwenye eneo hilo na
walianza wawafatilia watu hao
waliohusika na tukio
hilo laujambazi wa
kutumia silaha hizo za
jadi
Kamanda
Kidavashari alisema katika msako
huo wa Jeshi la polisi siku hiyo hiyo walifanikiwa
kumtia mbaroni mtuhumiwa
mmoja aitwaye Juma
Athumani 23 Mkazi
wa Mtaa wa Tambukaleli Mjini hapa
Alisema baada
ya kumkamata mtuhumiwa
huyo mmoja jeshi
hilo bado linaendelea
kuwatafuta watuhumiwa
wengine saba ambao walishiriki kwenye
tukio hilo la ujambazi wa kutumia
silaha za jadi
Aidha alieleza
kuwa mtuhumiwa Juma Athumani
anatarajiwa kufikishwa Mahakamani
mara baada ya upelelezi wa
tikio hili utakapo
kuwa umekamilika ili sheria iweze
kuchukua mkondo wake wa sheria
0 comments:
Post a Comment